Wednesday, October 26, 2016

WCB WALIMUWAHI SHAA (SK MUSIK) NA KUMSAINISHA MSANII HUYU WA KIKE>>>>>>>>>>>

Label ya Shaa, SK Musik, ilizidiwa ujanja na Wasafi Records ya Diamond na kumwahi kumsainisha msanii wa huyu wa kike.Jina lake ni Zoccu. Mwaka jana 2015 alishiriki kwenye shindano la Tecno Own The Stage lililofanyika nchini Nigeria.
Akizungumzia wasanii aliowapata kwa ajili ya kuwasimamia kupitia label yake, Shaa alisema alimpata Zoccu lakini akachelewa na hatimaye kukuta mwana si wake.
Nilimpata bwana binti mmoja anaitwa Zoccu lakini nikawa kidogo nimechelewa chelewa nikawa namuambia mwakani mara nashangaa napita Wasafi Records namkuta Zoccu kashachukuliwa,” Shaa aliiambia Millard Ayo.
Shaa amesema sasa anao wasanii wawili, Myler na mwingine kutoka Tanga na mwakani ataanza kuwatambulisha rasmi.

HII NI PERFOMANCE YA ZOCCU KWENYE TECNO OWN THE STAGE:-

No comments:

Post a Comment