Monday, November 21, 2016

MACHAS OFFICIAL SITE,INAKUALIKA KUTIZAMA PICHA 12 ZA STENDI KUU YA MABASI YAENDAYO MIKOANI,YA MJINI MOROGORO "MSAMVU BUS TERMINAL"ILIVYO KWA SASA,BAADA YA UKARABATI WA TAKRIBANI MIAKA MIWILI,karibu>>>>>

 Upande wa kuingilia abiria kwenye stendi hiyo.
 Abiria wakisubiri usafiri.
 BASI LIKIWA LINAINGIA...
 Muonekano wa mbele wa stendi hiyo.
 UTARATIBU WA NAMNA YA KUINGIA STENDI HUMU UKIENDELEA
 BASI LIKITOKA GETI KUU KUENDELEA NA SAFARI,BAADA YA KUSHUSHA NA KUPAKIA ABIRIA


 MMOJA WA MAAGENT,AKITAFUTA ABIRIA


 
REPORT BY JULIE KAVISHE-JOURNALIST MACHAS BLOG:-
baada ya ukarabati wa takribani miaka miwili, hatimaye Stendi ya Mabasi ya Mikoani ya Msamvu iliyopo Morogoro imefunguliwa mwishoni mwa wiki iliyopita huku ikiwa na muonekano wa kisasa kabisa na wengine kuifananisha na uwanja wa ndege Airport
BLOG YAKO PENDWA #MACHAS_OFFICIAL_SITE imefanikiwa kutinga ndani ya stendi hiyo ya kisasa ambayo iko kwenye hatua za mwisho za kumalizia ukarabati kwa kiwango cha hali ya juu, ambapo imeweza kupiga  picha  zinazoonyesha namna ambavyo mandhari ya stendi hiyo inavyovutia kwa sasa tofauti na ilivyokuwa awali kabla ya ukarabati.
blog yetu imeshuhudia abiria wengi wakipanda na kushuka kwenye mabasi kama ilivyoada lakini kwa sasa wakipanda na kushuka kama wako uwanja wa ndege kutokana na mandhari ilivyo vizuri mno kiasi cha kufananishwa na viwanja vya ndege(airport), huku wengine wakiwa wanasubiri usafiri ili kuelekea sehemu mbalimbali za ndani na nje ya nchi.
Akizungumza na reporter wa blog hii, mmoja wa viongozi wa Stendi hiyo, ameeleza kuwa, endapo wakimkamata mtu yoyote akiwa anatupa takataka ama kukanyaga bustani atatozwa faini ya Tsh. 50,000/= papo hapo.
 
PHOTOS & REPORT BY
 

No comments:

Post a Comment