Tuesday, June 20, 2017

MAAJABU:KIJANA ALIPA MAHARI BAADA YA MKEWE KUFARIKI>>>>>>>>

Kijana mmoja kusini mwa Msumbiji katika mkoa wa Inhambane alilazimika kumlipia mahari mkewe aliyefariki wikiendi iliyopita. Kulingana na chombo cha habari cha taifa msumbiji, mkewe alifariki kutokana na tatizo ya kujifungua.
Ndugu wa marehemu walimshutumu kijana huyo kwa kushindwa kuafiki majukumu yake ikiwemo kutambulishwa kwa jamaa na ndugu za mwanamke huyo kabla ya kufariki.
Ili kuhakikisha kuwa mazishi hayo yaliyozuiliwa yanafanyika, kijana huyo alilazimika kumnunulia nguo na viatu mkewe aliyefariki, kukubali kulipa zaidi ya dola 800 na kufanya harusi mnamo tarehe 15 mwezi Disemba.
Ndugu mmoja wa kijana huyo Irmao do Jovem alielezea kuwa walijaribu kuchangisha fedha zilizokuwa zinahitajika na waliweza kupata dola 178 pekee, na fedha zilizobakia walihaidi kulipa siku ya harusi....

No comments:

Post a Comment