Monday, July 4, 2016

KAULI YA CHADEMA KUHUSU UVUMI UNAOMUUSISHA NAIBU KATIBU MKUU WAKE MHESHIMIWA JOHN, JOHN MNYIKA



MHESHIMIWA JOHN MNYIKA, MBUNGE WA KIBAMBA PIA NAIBU KATIBU MKUU WA CHADEMA BARA
 
 
TAARIFA KWA UMMA

Ipo hoja nyepesi mno iliyopikwa na Vijana wa Lumumba juu ya Mbunge wa Kibamba na Naibu Katibu mkuu wa CHADEMA John Mnyika kuwa alimkataa Lowassa

Hoja hiyo ni ya kupuuzwa kwa kuwa haina ukweli wowote ule, na nitalishangaa Jeshi la Polisi kuendelea kukaa kimya,na kumuacha aliepotosha Umma kwa kiwango kikubwa kiasi hicho,jambo ambalo limempa Usumbufu mkubwa Naibu Katibu mkuu kwa chama na Wananchi wake katika jimbo lake.

Nataka kuona nguvu ya Cyber Crime kama kweli sheria hiyo ni dhahiri ni msumeno au huwa inakata upande mmoja tu!.Mnyika ni Kiongozi mkubwa na katika Taasisi kubwa sana nchini CHADEMA,hapaswi kunenewa uongo kwa nia ya kuupotosha Umma naliomba jeshi la Polisi liingie kazini Mara moja kutimiza majukumu yake.
 
Imetolewa July 03 Edward Simbeye
Katibu Mwenezi BAVICHA Taifa
 
 
$MACHAS OFFICIAL SITE
 




No comments:

Post a Comment