Sunday, July 3, 2016

Sallam Atoa Sababu ya Kuchelewa Kutoka kwa Video ya Wimbo wa Diamond na P-Square

DIAMOND PLATNUMZ- INTERNATIONAL ARTIST...
 
 
Diamond ana kesi ya kujibu kwa fans wake duniani pote. Ijumaa na Jumamosi hii wamekuwa wakisubiri kwa hamu video ya wimbo wake aliowashirikisha P-Square ambayo aliahidi angeitoa jana, lakini hadi sasa kimya!!

Wengi wameonesha kukosa uvumilivu na wameanza kuelezea kusikitishwa kwao kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii.

Lakini tumeongea na uongozi wake kutaka kujua nini sababu za kuchelewa kutoka kwa video hiyo, na umesema kuwa kuna vitu vichache vimechelewesha na kwamba mashabiki wasiwe na shaka kwasababu kiu yao itakatwa.

“Kuna vitu vinachelewesha ila tupo katika final touches,” meneja wa Diamond, Sallam ameiambia Bongo5.
“Ukiwapa kitu kibaya watalalamika ni bora wafanye subira wapate kizuri zaidi,” ameongeza.

Video ya wimbo huo ilifanyika nchini Afrika Kusini na utakuwa wimbo wa kwanza P-Square wanasikika wakiwa pamoja tangu kundi lao kudaiwa kuvunjika.

Ijumaa hii Diamond alipost kwenye Instagram picha ya mwanae Tiffah mwenye umri wa miezi 11 sasa na kuandika:" On the LONG conversation with my Miss World before Making a History.”
Ujumbe huo uliwapa matumaini mashabiki wake kuwa muda wa kuiona video hiyo umekaribia.
 
 
 
#MACHAS OFFICIAL SITE

No comments:

Post a Comment