Tuesday, May 10, 2016

Tyra: Kuwa mama kunanifunza mengi

NEW YORK, MAREKANI

MWANAMITINDO maarufu nchini Marekani, Tyra Banks, amesema tangu apate mtoto wake wa kwanza anaendelea kujifunza mengi kama mama wa familia.
Mrembo huyo alifanikiwa kupata mtoto wake wa kwanza wa kiume Januari mwaka huu na kumpa jina la York Banks na baba wa mtoto huyo anajulikana kwa jina la Erik.
“Nilikuwa nasikia sherehe za siku ya mama duniani, lakini mwaka huu nimekuwa na bahati kuwa miongoni mwa washerekeaji wa siku hiyo, ninaamini hadi sasa nimejifunza mengi kwa kipindi hiki.
“Kama nisingekuwa mama nadhani bado ningekuwa napitwa na mambo mengi, natumia nafasi hii kumshukuru mama yangu na mama wote kwa kusherehekea siku ya mama duniani, nawapenda sana,” aliandika Tyra.

No comments:

Post a Comment