Friday, May 13, 2016

Mwanamuziki Linah Asimulia Jinsi Alivyotumia Simu Kusaka Mpenzi



 
 
 

Msanii wa Bongo fleva Linah a.k.a ndege mnana amefunguka moja kati ya vitu ambavyo hawezi visahau katika maisha yake yote.

Akizungumza na Enewz Linna alisema kwamba moja ya kitu hicho ni tukio ambalo walilifanya yeye na mwenzie kipindi wanasoma kwani walikuwa wana tabia ya kujaribu kupiga namba tofauti tofauti ili kutafuta mpenzi.

“Nilifanikiwa kumpata mwanaume ambae nikawa ninawasiliana nae lakini siku tunaenda kuonana nae tulikutana na kitu hicho ambacho siwezi kusahau maana tulikutana na mtu ambae hatukutegemea kutokana na sauti yake ambavyo tulikuwa tukiisikia katika simu tukaamua kutojitokeza “,alisema Linna.
MSANII WA MUZIKI BONGO "LINAH SANGA"






No comments:

Post a Comment